Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Teknolojia mpya ya ‘Offside’ kutumika WC Qatar

Ijumaa , 1st Jul , 2022

Shirikisho la Soka Duniani ‘FIFA’ limethibitisha kuwa litatuma teknolojia mpya yenye utaalam wa hali ya juu ya kutambua mchezaji atakayeotea ‘Offside’ kwenye michuano ya kombe la Dunia inayotaraji kuanza Novemba 21, 2022 Nchini Qatar.

Gianni Infantino - Rais wa FIFA

Teknolojia hiyo itahusisa uwepo wa ‘sensor’ yaani kifaa maalumu cha kuhisi kitu kitakachowekwa ndani ya mpira huku kikiwa na uwezo wa kutuma taarifa mara 500 kwa sekunde kwa kusoma uelekeo halisi wa mpira.

Mbali na ‘Sensor’, lakini kutakuwa na kamera maalumu 12 ambazo zitawekwa kwenye kila paa la uwanja kwa ajili ya kufuatilia mwendo wa kutoka kwenye mwili wa kila mchezaji kwa kutuma taarifa mara 50 kwa sekunde kwa mchezaji aliye na mpira kwa wakati husika.

Mchezaji yeyote akiwa kwenye nafasi ya kuotea ‘Offside’ taarifa ya tahadhari itatumwa katika chumba cha waamuzi wasaidizi kwa njia ya video ambapo waamuzi hao watatuma taarifa haraka kwa mwamuzi wa kati ili imsaidie afanye maamuzi.

Mfumo huo ulijaribiwa katika michezo ya kombe la Dunia la vilabu msimu wa mwaka jana ambapo ilikadiriwa kupunguza muda uliokuwa unatumiwa na VAR kufanya maamuzi ya ‘Offside’ kutoka sekunde 70 hadi sekunde 25.

Upande wa mkuu wa waamuzi wa FIFA, Pierluigi Collina alisema mfumo huo ni mzuri na sasa uko tayari kwa ajili ya kutumika na waamuzi. Michuano hiyo mikubwa ya soka Duniani itaraji kuanza 21 Novemba 2022 na kutamatika Desemba 18, 2022 nchini Qatar.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi