
Maafisa wa CAF wakichezesha droo hiyo jijini Cairo Misri.
Akiongea mapema leo Oktoba 31, 2018, wakati anataja kikosi kitakachoingia kambini kwaajili ya kujiandaa na fainali hizo, kocha wa timu hiyo Boniface Pawasa amesema wamepangwa kundi gumu lakini haiwakatishi tamaa.
''Tumepangwa kundi gumu sana ambalo lina bingwa mtetezi Senegal pamoja na Nigeria ambaye alicheza fainali na Senegal hivyo sisi tutakuwa timu ndogo kwenye kundi hilo lakini tutajiandaa kwaajili ya kushindana na kuhakikisha tunafanya vizuri'', amesema Pawasa.
Mbali na Senegal pamoja na Nigeria pia kuna timu ya Libya katika Kundi B. Kundi A lenyewe lina timu za Misri, mabingwa wa zamani Madagascar, Morocco na Ivory Coast.
Michuano hiyo itafanyika nchini Misri kuanzia Desemba 8-14, 2018 katika fukwe za mjini Sharm El Sheikh.
Wachezaji walioitwa:
Ibrahim Abdallah
Ahmed Juma
Juma Ibrahim
Roland Msonjo
SAMWEL Salonge
Yahya Tumbo
Jarubu Juma
Ahmada Ahmada
Sudi Ame Sudi
Alphat Ndise
Kashiru Salum
Musa Hassan Mgosi
Ally Humud
Mohamed Makame
Shaffih Mussa
Justine Antony
Seif Mwinyi
Juma Kaseja