Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba yatuma salamu kwa Yanga

Jumamosi , 21st Oct , 2017

Klabu ya soka ya Simba imeendelea kuongoza msimamo wa ligi kuu soka Tanzania Bara baada ya kufanikiwa kuiadhibu Njombe Mji mabao 4-0 kwenye mchezo wa raundi ya 7 uliomalizika jioni hii kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Katika mchezo huo Simba ilianza kwa kushambulia lakini Njombe Mji walijitahidi kuwadhibiti washambuliaji wa Simba hadi dakika ya 28 ambapo mshambuliaji Emmanuel Okwi alifanikiwa kuiandikia Simba bao la kuongoza ambalo lilidumu hadi mapumziko.

Kipindi cha pili Simba walirejea kwa kasi na kuliandama lango la Njombe Mji ambapo katika dakika ya 51, kiungo Mzamiru Yassin alifanikiwa kufunga bao la pili kabla ya kuongeza bao la tatu dakika ya 52. Simba iliendelea kushambulia na kufunga bao la nne kupitia kwa Laudit Mavugo.

Simba sasa inaongoza ligi ikiwa na alama 15 sawa na Mtibwa Sugar ambayo nayo imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons. Azam FC imetoka sare ya 0-0 na Mbao FC wakati Lipuli FC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Majimaji FC. Matokeo mengine Ndanda FC imetoka sare ya 0-0 dhidi ya Singida United.

Emmanuel Okwi sasa amefikisha mabao 8 akiwa anaongoza orodha ya wafungaji msimu huu. Baada ya mchezo wa leo Simba itaelekea visiwani Zanzibar kujiwinda na mchezo dhidi ya watani wao wa jadi Yanga wikiendi ijayo.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali