Akizijibu tuhuma kuhusu Klabu ya Simba kujiendesha kwa hasara huku ikijua wazi haina vyanzo vingine vya mapato, Manara amesema kuwa kwa Tanzania klabu karibu zote zinajiendesha kwa hasara.
"Hakuna Klabu isiyojiendesha kwa hasara hapa nchini hilo linajulikana na siyo kwa Simba tu. Tunafanya mipango mingi kwa ajili ya kujikwamua katika hili. Siyo kweli kwamba Simba imetumia gharama kubwa za usajili kwa kuwa kuna pesa za Dewji. Muda mrefu tumekuwa tukifanya usajili wa aina hii sasa sifahamu hayo maneno yametoka wapi" Manara.
Katika hatua nyingine Manara amekanusha minong'ono yakwamba Mfanyabiashara huyo akijitoa Simba itashindwa kusimama imara.