
Mashabiki wa Simba uwanjani
Msemaji wa Simba Haji Manara amesema, mkutano huo umeitishwa baada ya kikao cha kamati ya utendaji wa klabu hiyo iliyokaa Novemba 18 mwaka huu.
“Kamati ya utendaji imetoa baraka zake kupitia ibara ya 22 ya katiba ya Simba na mkutano huo utakuwa ni muendelezo wa mkutano wa kawaida uliofanyika Julai 31 mwaka huu” amesema Manara.