Jumanne , 31st Oct , 2023

Saudi Arabia inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia la 2034 mara baada ya Australia kuamua kutowasilisha ombi la kutaka kuandaa mashindano hayo.

Saudi Arabia ndio taifa pekee ambalo limewasilisha ombi la kuandaa mashindano hayo kwa mwaka 2034. Kombe la Dunia la mwaka 2026 litafanyika Marekani, Mexico na Canada, huku kombe la dunia la mwaka 2030 lenyewe litafanyika katika nchi za Morocco, Ureno na Uhispania na pia baadhi ya mechi zitachezwa nchini Argentina, Paraguay na Uruguay.