Jumanne , 17th Feb , 2026

Chukua ujumbe huu kutoka kwenye ujumbe wa msanii wa Afrobeat kutoka nchini Nigeria Ayra Starr alipokuwa akifanya mahojiano huku nchini Marekani.

"Vitu ambavyo sio vya kuzingatia ni mawazo na mtazamo wawatu juu yako hivyo acha kuwaza ni namna gani watu wanakuchukulia maana watu wapo busy na maisha yao'' amesema Ayra Starr

''Uko busy unawaza vipi hawa watu wanawaza nini kuhusu mimi kumbe wao wanawaza ni namna gani wanaweza kusolve matatizo yao yanayowakumba, kuna mambo mengi sana watu wanapitia kwenye maisha yao hivyo acha kukaa na kuwaza watu wanakuonaje au wanakuchukuliaje'' amesema Ayra Starr

"Jitahidi kuwa wewe pambana ujipate na usijali kuhusu matokeo usiogope kufeli wewe feli mara nyingi unavyoweza lakini siku utakayopatia utafurahi na kujiona kuwa wewe ni wa thamani'' amesema Ayra Starr