Ijumaa , 20th Nov , 2015

Robo fainali ya michuano ya wavu ufukweni Mkoa wa Dar es salaam inatarajiwa kuendelea hapo kesho kwa timu za wanawake kupigwa michezo minne kwenye viwanja vya JK Park Kidongo Chekundu jijini Dar es salaam.

Mjumbe wa kamati ya mashindano ya Chama cha Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es salaam DAREVA, Nassor Sharrif amesema, ligi hiyo itaendelea Jumapili kwa timu za wanaume ambapo Jeshi Stars watacheza na Tanzania Prisons wakati IP Sports wataumana na Chui kwenye viwanja hivyo.

Sharrif amesema, michuano hiyo itakamilika wiki ijayo kwa hatua ya fainali ambapo wanaamini bingwa ataweza kuwakilisha vizuri mkoa katika mashindano mbalimbali.