Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Real Madrid yaweka rekodi mpya Hispania

Ijumaa , 13th Jan , 2017

Klabu ya Real Madrid imeweka rekodi mpya katika soka la Hispania kwa kucheza michezo 40 bila kupoteza baada ya kulazimisha sare ya 3-3 dhidi ya Sevilla katika mchezo wa Kombe la Mfalme uliopigwa usiku wa kuamkia leo.

Real Madrid wakishangilia bao la Asensio

 Sare hiyo ilipatikana kwa bao la Karim Benzema la dakika ya 93 na kuipiku Barcelona yenye rekodi ya kucheza mechi 39 bila kupoteza.

Mabao mengine ya Real Madrid yalifungwa na Sergio Ramos na Asensio na kuifanya ifuzu hatua ya robo fainali kwa jumla ya mabao 6-3.

Kipigo cha mwisho kwa timu hiyo chini ya Kocha Mkuu Zinedine Zidane kilikuja Aprili mwaka jana wakati timu hiyo ilipopoteza mechi ya kwanza ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya Wolfsburg ya Ujerumani na tangu wakati huo, haijafungwa mechi hata moja katika mashindano yote.

Barcelona ndio klabu ambayo walikuwa na rekodi ya zamani ya kucheza michezo 39 bila kupoteza mechi hata moja na timu hiyo, maarufu kama The Catalans, waliweka rekodi hiyo chini ya meneja Luis Enrique kati ya 2015 na 2016.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali