
Kocha Nuno Esoirito Santo
Nuno Espirito Santo ataondoka Wolves baada ya mchezo wa mwisho wa Jumapili wa msimu dhidi ya Manchester United. Bosi huyo wa Ureno anaondoka kwa kukubaliana baada ya miaka minne ya uongozi ambao ameongoza klabu hiyo kupanda ligi kuu ya England na kumaliza ligi katika nafasi ya saba, kabla ya kua na msimu usiokuwa na matokeo ya kuridhisha kwa upande wao.
Nuno sasa ameanza kutajwa kama kipaumbele katika nafasi ya kuchukua mikoba ya jose mourinho katika klabu ya Tottenham msimu ujao.