Jumapili , 19th Jun , 2016

Utemi wa Nico Rosberg kwa dereva mwenza wa Mercedes, Lewis Hamilton umezidi kuendelea baada ya kumgaragaza tena kwenye mashindano ya Europian Grand Prix, na kuzinyakua pointi 24 kutoka kwa bingwa huyo wa dunia.

Nico Rosberg akiruka juu kwa furaha mbele ya mshindi wa pili Sebastian Vettel (kushoto) na Sergio Perez

Nico Rosberg ametwaa taji la Europian Grand Prix, huku Dereva mwenza wa timu ya Mercedes, Lewis Hamilton akimaliza nafasi nafasi ya 5.
Rosberg aliongoza toka hatua ya mwanzo na kushinda taji la tano la formula 1 kwa msimu huu huko mji wa Baku, Azerbaijan.

Kushindwa kwa Hamilton, kunamfanya apoteze pointi 24 kwa Rosberg.

"Wikiendi iliisha vizuri".' Ilikuwa ya kushangaza, hivyo ninafuraha sana. Naburudika na ushindi huu, sherehe kubwa". Alisema Roseberg.