Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ni fainali ya kihistoria Kombe la Shirikisho

Jumamosi , 27th Mei , 2017

Simba SC ya Dar es Salaam na Mbao FC ya Mwanza leo zinakutana Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kwenye fainali za kuwania Kombe la Shirikisho l katika mchezo utakaoanza saa 10.00 jioni.

Tayari timu zote ziko mjini Dodoma na zimekuwa zikirushiana tambo za hapa na pale, wakati Simba wakiwa wamekamia kutwaa kombe hilo ili kujihakikishia ushiriki katika miachuano ya Kimataifa ambayo imeikosa kwa miaka takriban mitano.

Kwa upande wa Mbao, wao wanataka kuweka historia mpya katika soka la Tanzania kuwa timu ya kwanza kupanda daraja kwa 'Mlango wa Nyuma' na kisha kufuzu michuano ya Kimataifa.

Mbao FC pia inawania kuwa timu ya pili ya Mwanza kupata tiketi ya kucheza michuano ya Afrika, baada ya Pamba SC kufanya hivyo miaka ya nyuma.

Mchezo wa leo unatarajiwa kuchezeshwa na Ahmed Kikumbo wa Dodoma, atakayesaidiwa na Mohammed Mkono wa Tanga na Omary Juma wa Dodoma wakati mwamuzi wa akiba ni Florence Zablon pia wa Dodoma na Kamisaa ni Peter Temu wa Arusha.

Mshindi wa mchezo wa fainali (Kwa msimu huu kati ya Simba na Mbao), ndiye akayekuwa Bingwa wa Kombe la ASFC - HD, atapewa Kombe la Ubingwa na zawadi ya fedha kiasi cha shilingi milioni hamisini (50,000,000/-) kama zilivyoainishwa kwenye waraka wa zawadi wa michuano.

Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana Aprili 10, mwaka huu Simba ilitoka nyuma kwa mabao 2-0 na kushinda 3-2 ndani ya dakika 10 za mwisho katika mchezo wa Ligi Kuu Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza hiyo ilifanya Simba iwe imeifunga Mbao katika mechi zote za msimu, mechi zote zilizozikutanisha timu hizo kihistoria, baada ya Oktoba 20, mwaka jana kushinda pia 1-0 katika mchezo wa mzunguko wa kwanza Uwanja wa Taifa.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali