Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwandembwa kuwa pilato Kariakoo Derby, Mei 8

Jumanne , 4th Mei , 2021

Bodi ya ligi imemtangaza Emmanuel Mwandembwa ndiye atakayekuwa mwamuzi wa kati katika mchezo wa ligi kuu wa Mei 8, 2021 wa watani wa jadi, Simba dhidi ya Yanga utakaochezwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa Jijino Dar es Salaam.

Mwamuzi wa kati, Emmanuel Mwandembwa aliyechaguliwa kuuchezesha mchezo wa watani wa jadi wa Simba dhidi ya Yanga.(wa pili kutoka kulia)

Mwandembwa atashirikiana na mwamuzi msaidizi namba moja, Frank Komba kutoka Dar es Salaam aliyetwaa tuzo ya mwamuzi msaidizi bora msimu uliopita, mwamuzi msaidizi namba mbili, Hamdani Saidi wa mkoani Mtwara.

Mwamuzi wa kati bora wa msimu uliopita wa VPL, Ramadhani Kayoko amechaguliwa kuwa mwamuzi wa akiba wa mchezo huo unatazamiwa kuwa wenye upinzani mkali kutokana na Utamaduni wa utaji wa jadi lakini pia kutokana na presha za kuwania ubingwa wa ligi kuu.

Ikumbukwe hii si mara ya kwanza kwa Emmanuel Mwandembwa kuwa pilato wa mchezo huo mkubwa nchini na Afrika kiujumla, kwani msimu wa mwaka 2018 aliamua mchezo huo kwa kuonesha kuumudu vema.

Mwandembwa pia ana uzoefu wa kiasi wa kusimamia mchezo wa kimataifa kwani Agosti 11,  2019 alikuwa mwamuzi wa akiba kwenye mchezo wa klabu bingwa Afrika kati ya Aigle Noir ya Burundi dhidi ya wababe wa Kenya, Gor Mahia huku Elly Sasii wa Tanzania akiwa mwamuzi wa kati.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali