Mo Dewji na Mbwana Samatta
Mchezo huo ulimalizika kwa Aston Villa kupoteza kwa mabao mawili kwa moja, huku bao la Aston Villa likifungwa na Mbwana Samatta katika dakika ya 41 ya mchezo.
Malalamiko ya mashabiki wengi wa Tanzania hasa katika mtandao wa Twitter ni juu ya mchezaji huyo kutopewa alama ya blue 'Verification' kutoka kwa mtandao huo na miongoni mwao ni bilionea na mwekezaji wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji 'Mo' ambaye kupitia ukurasa wake wa Twitter amemuomba mmoja wa wahusika wa masuala ya teknolojia katika mtandao huo kumpa 'Verification' Samatta kwakuwa ni mtu maarufu Tanzania.
Hey @jack,
Can kindly verify @Samagoal77_’s account? He’s made history as the first Tanzanian to:
Win the African CL
Score in the #UEL
Score in the #UCL
Play & score in the #PL
Score in the #CarabaoCupFinalSincerely,
Tanzanian’s on Twitter
(#TOT) pic.twitter.com/7va8xnUtjz— Mohammed Dewji MO (@moodewji) March 2, 2020
