Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mnyama afanya kweli, atinga nusu fainali

Jumapili , 19th Mar , 2017

Bao pekee la mshambuliaji Laudit Mavugo raia wa Burundi limetosha kuivusha Simba SC hadi hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho, baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Madini SC.

Laudit Mavugo katika moja ya mechi zake

Katika mechi hiyo ya robo fainali iliyopigwa katika dimba la Sheikh Amri Abeid Arusha, Simba licha ya kushusha 'full muziki' katika kikosi chake, imekutana na ushindani mkali kutoka kwa vijana hao wa Madini inayoshiriki ligi daraja la pili, kiasi cha kumaliza dakika 45 za kipindi cha kwanza bila bao kwa kila upande.

Safu ya ushambuliaji ya Simba iliyoongozwa na Ibrahim Ajib na Laudit Mavugo iliyosaidiwa kwa ukaribu na Shiza Kichuya na Mohamed Ibrahim ilishindwa kutumia nafasi kadhaa ilizopata licha ya kukosekana kwa pasi makini za mwisho, huku vijana wa Madini pia wakiwa hawana uoga wowote na kuonesha uwezo mkubwa wa kumiliki mpira na kuifanya mashambulizi.

Ilikuwa ni dakika ya 54 ya mchezo ambapo Mavugo alitumia udhaifu wa beki wa Madini aliyeshindwa ku-'control' mpira wa juu uliomfikia akiwa kama beki wa mwisho, na Mavugo kumzidi uwezo na kuunganisha kwa kichwa kilichompita golikipa wa madini aliyekuwa mbali kidogo na goli.

Juuko Murshid

Katika mechi ya leo safu ya ulinzi ya Simba imeongozwa na Mganda Juuko Murshid ambaye hajaonekana kikosini tangu mwaka jana kutokana na matatizo aliyokutana nayo ikiwemo msiba pamoja na kushiriki michuano ya AFCON.

Murshid mwenyewe anasema anaamini kuwa uwezo wake unamruhusu kuwa sehemu ya kikosi cha kwanza, hivyo atajitahidi kumshawishi mwalimu kwa njia ya mazoezi na bidii awapo uwanjani

Kwa matokeo hayo, Simba inaungana na Mbao FC ya Mwanza katika hatua ya nusu fainali, huku timu nyingine mbili zikisubiriwa.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali