Akizungumza jijini Dar es salaam, Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania TPBO Yassin Abdallah Ustaadh amesema,wameamua kumleta bondia Mganda ambaye ni namba moja ili kuleta changamoto kwa Miyeyusho.
Ustaadh amesema, katika mapambano ya kesho Mada Maugo atapanda ulingoni kupambana na Jackob Maganga kuwania Ubingwa wa UBO ukanda wa Afrika huku Kalama Nyilawila akipambana na Allybaba Ramadhani.