Jumamosi , 13th Mei , 2017

Kwa jinsi hali ilivyo mpaka sasa, Amissi Tambwe anaamini kwa asilimia 100 kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu atatokea Yanga.

Amissi Tambwe

Kwa mujibu wa Tambwe, anapata nguvu ya kusema hayo kutokana na ukweli kwamba, kikosi chao ndipo wanapotokea wachezaji wengi wanaojua kufunga.

Mpaka wakati huu Simon Msuva (Yanga) ana mabao 13 akifuatiwa na straika wa Ruvu Shooting, Abdulrahman Mussa mwenye mabao 12.

Obrey Chirwa wa Yanga, Mbaraka Yusuph (Kagera Sugar) na Shiza Kichuya wa Simba wote wana mabao 11  pamoja na Tambwe .