Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mchenga wabakiza mechi moja kutetea ubingwa

Jumatano , 22nd Aug , 2018

Mabingwa watetezi wa michuano ya Kikapu ya Sprite Bball Kings Mchenga Bball Stars wameendelea kujiweka vizuri kwenye mbio za kutetea ubingwa wao walioutwaa mwaka 2017 baada ya kushinda game 2 kwa pointi 85 dhidi ya 65 za Flying Dribblers.

Wachezaji wa Mchenga Bball Stars na Flying Dribblers kwenye game 2.

Matokeo hayo sasa yamewafanya Mchenga Bball Stars kushinda game mbili mfululizo kwenye 'best of five' ya fainali ya Sprite Bball Kings baada ya kushinda game 1 iliyopigwa Agosti 18 kwenye uwanja wa taifa wa ndani.

Katika mchezo wa leo uliopigwa kwenye viwanja vya Don Bosco Oysterbay mchezaji Baraka Sadick wa Mchenga ameendelea kuwa moto wa kuotea mbali baada ya kuongoza kwa pointi katika game 1 na leo kufanya hivyo tena akifunga pointi 28 kati ya 85 za Mchenga Bball Stars. 

Pia amechukua rebound 9 na kutoa Assist 5. Kwa upande wa Flying Dribblers mchezaji Steve Mtemihonda, amefunga pointi 19 na kuchukua rebound 6 pamoja na kutoa Assist 2. 

Game 3 ya 'best of five' itapigwa Jumamosi Agosti 25, kwenye uwanja wa ndani wa taifa, ambapo kama Mchenga watashinda watatetea ubingwa wao rasmi lakini kama Flying Dribblers watasawazisha basi itasubiriwa game 4.
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu