Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Matola aondoka Simba SC

Jumatatu , 14th Nov , 2022

Uongozi wa Klabu ya Simba umethibitisha kuwa Kocha wao Msaidizi wa Simba, Seleman Matola ataondoka kwenye benchi la ufundi la timu hiyo kwa muda kwaajili ya kwenda kwenye kozi ya Ualimu ya leseni A ya CAF, itakayoanza Novemba 21 mwaka huu.

Taarifa hiyo imethibitishwa na Meneja wa Mawasiliano Simba SC, Ahmedy Ally ambaye amesema, wanafurahi kwa hatua hiyo kwani Matola akiimaliza kozi hiyo basi atakuwa atapanda daraja na kuruhusiwa kuwa Kocha Mkuu katika vilabu vya Ligi kuu.

''Ni kweli tumepokea maombi kutoka kwake na hii ni fursa kwake kwenda kujiongeza katika idara ya elimu , sisi Simba tunamtakia kila la kheri'' amesema Ahmedy Ally.

Mabosi wa Simba watalazimika sasa kuboresha benchi la ufundi kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma kocha huyo alipokwenda kusoma timu ikiwa chini ya Didier Gomes ambapo alitafutiwa msaidizi wake Thierry Hitimana na baadaye Matola aliungana nao alipomaliza masomo yake.

Simba inatarajiwa kushuka dimbani Jumatano ya Novemba 16 mwaka huu kucheza mchezo wa Ligi Kuu NBC Tanzania dhidi ya Namungo katika uwanjna wa Benjamin Mkapa majira ya saa moja usiku .
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali