Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manchester City yanyooshewa mikono na wapinzani

Alhamisi , 18th Feb , 2021

Kocha wa Everton Carlo Ancelotti ameipongeza Manchester City na kuweka wazi kuwa timu hiyo ni imara kwenye kila idara, baada ya kikosi chake kupoteza kwa mabao 3-0 usiku wa jana, kwenye mchezo wa ligi kuu England na ushindi huo unaifanya Man City kuongoza ligi kwa tofauti ya alama 10.

Manchester City wameshinda michezo 12 mfululizo ya ligi kuu England

Vinara wa EPL Manchester City wametengeneza tofauti ya alama 10 kati yao na majirani zao Manchester United wanaoshika nafasi ya pili, baada ya matajiri hao wa jiji la Manchester kushinda mchezo wao wa 12 mfululizo kwa kuinyuka Everton mabao 3-0.

Kufuatia kikosi chake kukubali kipigo hicho kocha wa Everton raia wa Italia Carlo Ancelotti, alisistiza kuwa Man City ni timu imara kwa sasa.

''Man City, katika wakati huu, wako katika hali nzuri. Wana ubora mzuri, wana imani, wana nguvu. Tulijaribu kufanya kila jitihada lakini ilikuwa ngumu, dhidi ya Rodrigo, Ruben Dias, dhidi ya Aymeric Laporte.''

Mabao ya Manchester City yalifungwa na Phil Foden, Riyad Mahrez, na Bernardo Silva na lile la Everon lilifungwa na Richarlison, huu ni ushindi wa 17 kwa kocha Pep Guardiola na vijana wake kwenye mashindano yote na sasa wamefikisha alama 56, wakiwa wanaongoza kwa tofauti ya alama 10 dhidi ya Manchester United wenye alama 46 walio nafasi ya pili.

 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA