
Katika mchezo mwingine utakaopigwa hapo kesho, wajelajela Tanzania Prisons wakiwakaribisha African Sports katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Afisa Habari wa Klabu ya Azam FC Jaffary Iddy Maganga amesema, mchezo utakuwa mgumu kwani JKT Ruvu ni wazuri na ni wapinzani kwa muda mrefu.
Maganga amesema, majeruhi waliokuwa nao ambao ni Mudathir Yahya na Farid Mussa hivi sasa wanaendelea vizuri, hivyo kupangwa katika mchezo huo itategemea na kocha huku kocha mkuu Stewart Hall akiwa na kikosi chake uwanjani hapo kesho baada ya kumaliza adhabu ya kadi aliyokuwa akiitumikia.