Jumapili , 20th Jun , 2021

Timu ya vijana ya Mtibwa Sugar wenye umri wa chini ya miaka 20,wamefanikiwa kutwaa ubingwa ya mashindano ya vijana kwa timu za ligi kuu iliyomalizika jumamosi hii katika uwanja wa Chamazi baada ya kuwafunga Yanga-U20 kwa magoli 2-1.

Mfungaji bora wa mashindano hayo Omary Marungu akifunga goli la kwanza

Mtibwa wametwaa ubingwa  huu kwa mashindano ya vijana kwa timu za ligi kuu , kwa mara ya pili mfululizo baada ya kufanya hivyo mwaka jana kwa  kuwafunga  Azam U-20 kwa  penati  4-2 baada ya kwenda  suluhu kwa dakika 120

Timu hiyo ya vijana imekuwa inafanya vizuri miaka ya karibuni,tofauti sana na timu yao ya wakubwa ambayo kwa mara ya mwisho  ilitwaa ubingwa  miaka  21  iliyopita,misimu miwili hii imekuwa katika hatari  kubwa  ya kukaribia  kuporomoka daraja.

Maswali ni mengi wapi Mtibwa wanafanikiwa , kuna siri gani iliyofichika ndani yake? ni kweli  timu za vilabu vya Simba Yanga na Azam zimeshindwa kupata muarobani wa kupambana nayo, kuna uwekezaji gani tofauti kwenye timu za vijana hadi kupata mafanikio hadi kuwafanya watwae  ubingwa mfululizo.

Timu hiyo ya Mtibwa U-20 pia ilijizolea tuzo nyingi za mashindano  hayo kama kocha bora iliyokwenda kwa Awadh Juma, Omary Marungu akipata ya  mfungaji bora,   Jojo Mkele alitajwa  kuwa  kiungo bora wa mashindano pamoja  na mchezaji bora wa ujumla.