Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kocha wa zamani wa Yanga aomba kazi Singida United

Jumamosi , 26th Mei , 2018

Baada ya hivi karibuni kuongea na East Africa Television na kuthibitisha kuwa wanaachana na kocha wao Hans Van Pluijm, Mkurugenzi wa Singida United Festo Sanga, leo ameweka wazi kuwa wamepokea maombi ya kocha wa zamani wa Yanga Dusen Kondic.

Sanga amesema bado wanapitia wasifu wa makocha mbalimbali kutoka maeneo tofauti ambao wameomba kuchukua mikoba ya Hans ambaye anaondoka klabuni hapo baada ya mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Mtibwa Sugar Juni 2.

''Mpaka sasa hatuna uhakika wa nani atachukua nafasi ya Hans, lakini tutatangaza hivi karibuni baada ya watalaam wetu wa masuala ya ufundi kumaliza kazi ya kupitia majina yaliyoomba kazi, akiwemo kocha wa zamani wa Yanga Mserbia Dusen Kondic pamoja na wengine wa nje na hapa kwetu'', amesema.

Dusen Kondic alijiunga na Yanga November 2007, akichukua mikoba ya Mserbia mwenzake Sredejovic 'Micho' Milutin.  Hata hivyo hakudumu ndani ya klabu hiyo kwani alifutwa kazi mwishoni mwa msimu wa 2007/08.

Singida United ambayo imerejea ligi kuu msimu huu, imeonesha ushindani mkubwa ambapo hadi sasa ipo katika nafasi ya 5, ikiwa imesalia mechi moja kumalizika kwa msimu. Timu hiyo pia inaweza kupata nafasi ya kuwakilisha nchi endapo itaifunga Mtibwa Sugar kwenye fainali ya FA Juni 2.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi