Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kilichojiri, ufunguzi wa Sprite Bball Kings 2019

Jumamosi , 17th Aug , 2019

Michuano ya Sprite Bball Kings 2019 inayoandaliwa na EATV, EA Radio kwa kushirikiana na kinywaji cha Sprite imezinduliwa Jumamosi Agosti 17 katika viwanja vya Mlimani City.

Picha katika matukio ya jana

Huu ni msimu wa tatu wa michuano hiyo, ambapo katika usajili na ufunguzi, timu mbalimbali zimejitokeza kujisajili na kutakuwa na hatua za mtoano kisha robo fainali, nusu fainali na fainali.

Akifungua rasmi michuano, mwakilishi kutoka Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Malinde Lutiho Mahona amesema kuwa Serikali inatambua juhudi kubwa zinazofanywa na East Africa Tv, East Africa Radio na kampuni ya Coca-Cola kupitia kinywaji chake cha Sprite kwa moyo wao wa kujitolea kukuza mpira wa kikapu nchini.

"Serikali ipo pamoja na nyinyi, inatambua faida kubwa iliyopo kwenye michezo ndio maana inapoona watu wenye moyo kama Coca-Cola, East Africa Radio & East Africa Tv . Tunatoa pongezi sana", amesema Mahona.

"Pia tunawaomba wadau wengine wawekeze katika viwanda vya michezo ili tupate vijana ambao Taifa zima linawaangalia, kwahiyo kwa sasa vijana onesheni vipaji vyenu katika mashindano haya", ameongeza.

Naye kwa upande wake, Mkurugenzi wa Umma na Mawasiliano wa Coca-Cola ambayo inazalisha kinywaji cha Sprite, Haji Mzee Ally amesema, "ahadi yetu kama Coca-Cola ni kuendelea kuwa mstari wa mbele hasa linapokuja suala la kuwasaidia vijana, katika kuendeleza vipaji vyao ambavyo vitaleta mabadiliko katika maisha yao".

Akaongeza, "tumelidhihirisha zaidi kupitia majukwaa mengine ya kuibua vipaji kama vile Coke Studio Afrika, East Africa Got Talent na mashindano ya COPA Coca-Cola."

Mpaka zoezi la usajili linakamilika katika viwanja vya Mlimani City, jumla ya timu 39 zimeshajisajili kwa ajili ya michuano hiyo inayotarajia kutimua vumbi hivi karibuni. Zoezi la usajili litaendelea tena Jumatatu ya Agosti 19.

Aidha wimbo maalum wa michuano ya Sprite Bball Kings 2019 umezinduliwa katika siku ya uzinduzi hii leo ambapo wasanii waliofanya wimbo huo, G Nako 'Warawara', Frida Amani na Chemical, walipata nafasi ya kuuzindua rasmi mbele ya wageni waalikwa na watu waliojitokeza.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali