Jumanne , 29th Nov , 2016

Meneja wa timu ya Taifa ya Mpira wa Ufukweni Deo Lucas ametaja kikosi cha wachezaji 12 ambacho kitaingia kambini kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya Taifa ya Uganda mchezo utakaopigwa Desemba 9 mwaka huu jijini Dar es salaam

Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni

Ameongeza kuwa katika kikosi hicho walitakiwa wachezaji 13 lakini nafasi ya mlinda mlango bado ipo wazi na kocha anatarajia kumtangaza hivi karibuni.

Deo amesema, nafasi ya mlinda mlango ilikuwa ni ya Juma Kaseja lakini kutokana na kubanwa na ratiba imewabidi kuacha nafasi hiyo ili kuweza kuangalia mlinda mlango mwingine ambaye ataungana na kikosi ambacho kitaingia kambini Desemba Mosi mwaka huu.

Deo amewataja katika kikosi cha wachezaji 12 kitakachoingia kambini wachezaji watatu ni kutoka visiwani Zanzibar.

Wachezaji walioitwa kambini ni Rabi Ally Rabi, Rajab Gana, Halifa Mgaya, Loland Revocatus, Mwalimu Akida, Juma Ibrahim, Kashilu Salum, Mohamed Rajab, Twalib Ally, Ahmada Ally, Kassim Kilungo na Samuel John.