Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Kapambaneni kwa ajili ya taifa'' Msitha

Jumanne , 6th Dec , 2022

Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Neema Msitha ametoa wito kwa waogeleaji kwenda kupambana kufa na kupona Ili kufanye vizuri katika mashindano ya Dunia ambayo yanatarajia kuanza Disemba 13 hadi 19 mwaka huu nchini Australia.

Msitha ameyasema hayo leo Disemba 06, 2022 wakati akiwaaga na kuwakabidhi bendera waogeleaji wa timu ya Taifa watakaoiwakilisha nchi katika michuano hiyo ambao wanatarajia kuondoka Disemba 08 nchini kuelekea katika mashindano hayo.

Amewataka wachezaji hao kwenda kuitangaza Tanzania kupitia utamaduni wake, lugha ya kiswahili  na kuipeperusha bendera ya Taifa vyema pamoja na kuzingatia nidhamu.

"Leo tunawakabidhi bendera hii  na mnabeba jukumu la watanzania  kwa kuitangaza nchi na mkaipeperushe vyema bendera na sina mashaka na maandalizi yenu nawaamini, msiende kinyonge serikali tupo pamoja nanyi," amesema.

Msitha ameyaomba makampuni kujitokeza kuwekeza katika michezo mingine ukiwamo wa kuogelea Ili kutoa fursa sambamba na vyama vya michezo kuiga programu za kuibua vipaji ambavyo vitasaidia kuchagua wachezaji  bila upendeleo.

Naye Makamu wa Rais wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA) Asma Hilal, àmesema wachezaji wapo tayari kwenda kupambana  ili warudi na matokeo mazuri na ahadi kwa watanzania watafanya vizuri, huku akiwaomba watanzania kuwaombea dua na maombi timu iweze kufanya vizuri na kupeperusha bendera ya Taifa vyema.

Kwa upande wa Kocha wa timu hiyo Alex Mwaipasi ametaja wachezaji wanne watakaoiwakilisha nchi kuwa ni pamoja na Collin Saliboko, Hilal Hilal, Ria Save na Sophia Latiff.

Aliongeza kuwa wataendelea kutunza heshima na hayo mashindano ni kipimo chao cha Daraja la Kimataifa ikiwa kiu yao ni kufuzu kimataifa na walichofanya katika mashindano yaliyopita wataongeza .

Kwa niaba ya wachezaji Collins Saliboko, alisema wamejipanga vizuri  na lengo lao kuu ni kuhakikisha wanapunguza muda na kufikia olimpiki.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao