Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Kapambaneni kwa ajili ya taifa'' Msitha

Jumanne , 6th Dec , 2022

Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Neema Msitha ametoa wito kwa waogeleaji kwenda kupambana kufa na kupona Ili kufanye vizuri katika mashindano ya Dunia ambayo yanatarajia kuanza Disemba 13 hadi 19 mwaka huu nchini Australia.

Msitha ameyasema hayo leo Disemba 06, 2022 wakati akiwaaga na kuwakabidhi bendera waogeleaji wa timu ya Taifa watakaoiwakilisha nchi katika michuano hiyo ambao wanatarajia kuondoka Disemba 08 nchini kuelekea katika mashindano hayo.

Amewataka wachezaji hao kwenda kuitangaza Tanzania kupitia utamaduni wake, lugha ya kiswahili  na kuipeperusha bendera ya Taifa vyema pamoja na kuzingatia nidhamu.

"Leo tunawakabidhi bendera hii  na mnabeba jukumu la watanzania  kwa kuitangaza nchi na mkaipeperushe vyema bendera na sina mashaka na maandalizi yenu nawaamini, msiende kinyonge serikali tupo pamoja nanyi," amesema.

Msitha ameyaomba makampuni kujitokeza kuwekeza katika michezo mingine ukiwamo wa kuogelea Ili kutoa fursa sambamba na vyama vya michezo kuiga programu za kuibua vipaji ambavyo vitasaidia kuchagua wachezaji  bila upendeleo.

Naye Makamu wa Rais wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA) Asma Hilal, àmesema wachezaji wapo tayari kwenda kupambana  ili warudi na matokeo mazuri na ahadi kwa watanzania watafanya vizuri, huku akiwaomba watanzania kuwaombea dua na maombi timu iweze kufanya vizuri na kupeperusha bendera ya Taifa vyema.

Kwa upande wa Kocha wa timu hiyo Alex Mwaipasi ametaja wachezaji wanne watakaoiwakilisha nchi kuwa ni pamoja na Collin Saliboko, Hilal Hilal, Ria Save na Sophia Latiff.

Aliongeza kuwa wataendelea kutunza heshima na hayo mashindano ni kipimo chao cha Daraja la Kimataifa ikiwa kiu yao ni kufuzu kimataifa na walichofanya katika mashindano yaliyopita wataongeza .

Kwa niaba ya wachezaji Collins Saliboko, alisema wamejipanga vizuri  na lengo lao kuu ni kuhakikisha wanapunguza muda na kufikia olimpiki.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto