Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Giggs ajiengua Wales kuelekea kombe la Dunia

Jumanne , 21st Jun , 2022

Aliyekua kocha mkuu wa timu ya taifa ya Wales Ryan Giggs ametangaza kujiuzulu rasmi nafasi ya kukinoa kikosi chataifa hilo, baada ya kusimama kazi hiyo tangu mwezi Novemba 2020 akikabiliwa na kesi ya unyanyasaji wa kijinsia alioufanya nyumbani kwake jijini Manchester.

Ryan Giggs aliyekua kocha wa Wales

Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United mwenye umri wa miaka 48 alishutumiwa kumshambulia na kumnyanyasa mpenzi wake wa zamani Kate Greville kati ya mwezi Agosti 2017 na Novemba 2020, lakini Giggs amekanusha tuhuma hizo na kukana mashitaka yote.

Katika taarifa yake, Giggs alisema: "Imekuwa ni heshima na nafasi ya pekee kuisimamia nchi yangu, lakini ni vyema shirkisho la soka la Wales, timu ya wakufunzi na wachezaji kujiandaa kwa ajili ya michuano ya kombe la dunia kwa uhakika, bila kuwaza kuhusu nafasi ya kocha mkuu."

Baada ya kutoa taarifa hiyo, Chama cha Soka cha Wales FAW kimetoa shukrani zake kwa Ryan Giggs kwa muda wake aliokuwa kocha wa timu ya taifa ya wanaume na inaheshimu uamuzi ambao amechukua, kwa manufaa ya soka ya la Wales.

Muda wote ambao Giggs alienguliwa kikosini timu ya Wales ilikua chini kocha msaidizi Robert Page aliyeiongoza Wales kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza baada ya miaka 64 bila Giggs. Page ndiye ataoingoza pia timu hiyo nchini Qatar baada ya Giggs kuamua kujiuzulu.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi