
Kibadeni amesema CECAFA ilionyesha wazi ilitaka kuona Ethiopia wanafika mbali licha ya kuwa na kikosi kibovu.
Kibadeni amesema hakuwampanga Mlinda Mlango Aishi Manula pamoja na mshambuliaji Elius Maguli katika mechi ya pili ya Ethiopia hatua ya robo fainali kwa kuwa walikuwa na kadi mbili za njano huku Ally Mustapha Barthez naye akiwa mgonjwa.
Stars imewasili hapo jana ambapo ilimaliza mechi zote mbili dhidi ya Ethiopia kwa sare ya 1-1 lakini hatua ya robo fainali ikatolewa kwa mikwaju ya penalti 4-3.