Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chelsea, heri punda afe mzigo ufike

Ijumaa , 13th Jan , 2023

Todd Boehly anakaribishwa kwenye ulimwengu wa 'stress', licha ya pesa zake zote lakini moja ya kitu kinamnyima usingizi hivi sasa ni Chelsea, usajili bora anaendelea kuufanya lakini matokeo bado magumu, hiki kitu huwa kinawapa shida sana matajiri hasa kwenye biashara zao.

Kocha wa Chelsea, Grahm Potter na nahodha Cesar Azpilicueta

Mashabiki wengi wa Chelsea wanaamini angekuwepo bosi Roman Abramovich asingekubali kudhalilishwa namna hii. Wanakumbuka urejeo wa pili wa Jose Mourinho pale darajani, alishinda ubingwa wa ligi lakini baada ya mechi 18 za msimu uliofuata, Roman Abramovich akamla kichwa kabla ya sikukuu ya Christmas 2015 kwasababu yeye alikuwa mtu wa matokeo na ndiyo maana Chelsea imekuwa kubwa na kufikia hapa ilipo kuwa na mataji 2 ya Klabu Bingwa Ulaya kuizidi Arsenal na taji moja nyuma ya Man United.

Kama hiyo haitoshi msimu 2016/17 Chelsea ilishinda ubingwa wa EPL na FA Cup chini ya Antonio Conte, halafu niulize nini kilitokea msimu uliofuatia!!. Conte alitimuliwa kwa kuikosesha Chelsea nafasi ya kushiriki Klabu Bingwa Ulaya.

Kwenye miaka takribani 19 ya Abramovich pale Chelsea ameajiri makocha 13, lakini ndiyo timu yenye mafanikio makubwa ya ndani na nje, kutokana na mtazamo tu wa Abramovich. Bwana Todd Boehly  ameamua kuja na mfumo tofauti wa kuamini mipango ya muda mrefu, ndiyo maana hata bodi yake imekuja na kauli ya kumlinda kocha Graham Potter licha ya matokeo mabaya anayopitia.

Lakini tunamkumbusha kuwa hakuna kocha Muingereza aliyechukua ubingwa wa EPL tangu Sir Alex Ferguson alipofanya hivyo mwaka 2013. Ni yeye tu bwana Boehly kuamua 'Punda afe mzigo ufike' ili mashabiki waendelee kula burger au kuwa baridi kusubiri project ambayo itazaa matunda baada ya miaka kadhaa huku akiwalisha kisamvu cha kwetu Nakapanya !!

Imeandikwa na @manafi_daimu   
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu