Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Cannavaro atetea Yanga kufungwa

Jumapili , 13th Aug , 2017

Beki kisiki wa kati na nahodha wa timu ya Yanga Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema kujifunga kwa beki mpya wa timu hiyo hapo jana Abdallah Hajji ‘Ninja’  ni moja ya matukio ya mchezo na isitafsriwe kwamba beki huyo ni uchochoro au ana uwezo mdogo.

Cannavaro amesema 'Ninja' ni beki chipukizi mwenye uwezo mkubwa na kinachomkumba sasa hivi ni presha ya timu hiyo kutokana na kwanza ndiyo amesajiliwa na hakuwahi kucheza timu kubwa kama Yanga hivyo ana mambo ya kujifunza kwa wakati huu inabidi apewe muda ili azoee mazingira na baadaye matunda yake yataonekana.

Beki Hajji ‘Ninja aliyejifunga 

Cannavaro amesema hayo ikiwa ni siku moja tangu timu hiyo hapo jana jioni ipoteze mchezo wa kirafiki baada ya kufungwa bao 1-0 na Ruvu Shooting Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam ambapo beki Hajji ‘Ninja’ alimfunga kwa kichwa cha mkizi kipa wake, Ramadhan Awam Kabwili dakika ya 22 wakati akijaribu kuokoa krosi ya Shalla Juma kutoka upande wa kushoto wa Uwanja na kuipatia bao pekee la ushindi Ruvu Shooting.

Huo ulikuwa mchezo wa pili wa kujipima nguvu kwa Yanga inayofundishwa na kocha Mzambia, George Lwandamina baada ya Jumamosi iliyopita kushinda 3-2 dhidi yas Singida United Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Na baada ya matokeo hayo, Yanga SC imeondoka hii leo jijini Dar es Salaam mapema kwenda Zanzibar ambako usiku huu watamenyana na Mlandege Uwanja wa Amaan katika mchezo mwingine wa kirafiki.

Mapema kesho Jumatatu Yanga watakwenda kisiwani Pemba kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba Agosti 23 Uwanja wa Taifa. 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali