Boston Celtics wamefuzu fainali ya NBA kwa mara ya 22
Celtics wameshinda michezo 4 kwa 3 kwenye mfululizo wa michezo 7 ya fainali waliocheza na wataminyana na Golden state worriors kwenye mchezo wa fainali. Ni kwa mara ya 22 Celtics wanafuzu kucheza fainali ya NBA wao ni mabingwa mara 17 na mara ya mwisho kutwaa ubingwa ilikuwa mwaka 2008.
Katika mchezo huu wachezaji nyota wa Boston Celtics Marcus Smart amefunga alama 24, pasi za kufunga (Assists) 5 na amechukua rebound 9 nae Jayson Tatum amefunga alama 26, pasi za kufunga 6 na rebound 10.


