Bondia Kubrat Pulev akimpiga busu mwandishi.
Mwanadada huyo anayejulikana kwa jina la Andrea, akifanya mahojiano na moja kati ya chombo cha habari nchini humo, ameoneshwa kutoridhishwa na adhabu aliyopewa mpenzi wake na kuiita kuwa ni uonevu dhidi ya Bondia huyo.
"Hii ni adhabu mbaya sana kwake, kwani haya ndiyo maisha yake. Mimi sijaona kama kilikuwa kitu kikubwa hivyo kumfanyia hivi ni kumuua", amesema Andrea.
Tume ya michezo ya mji wa Calfornia, Marekani imetangaza kumfungia kushiriki pambano lolote kwenye mji huo hadi pale atakapojitokeza na kufanya mazungumza nao kuhusiana na hilo tukio.
Jenny Sushe, ambaye ndiye mwandishi wa habari aliyefanyiwa kitendo hicho pia amemfungulia mashtaka mahakamani mwanamasumbwi huyo.




