Jumatano , 14th Aug , 2024

Klabu ya Azam FC imethibitisha kuwa kiungo Adolf Mtasingwa Bitegeko (25) amesaini nyongeza ya mkataba mpya wa miaka miwili utakaombakisha kwa Waoka Mikate hao mpaka 2027.

Mkataba wa awali wa Mkata umeme huyo raia wa Tanzania ulikuwa utamatike Juni 2025 lakini sasa ataendelea kudumu kwenye viunga vya Azam Complex, Chamazi mpaka Juni 2027.