Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Arteta alia na Arsenal, kuwakosa watatu leo

Jumamosi , 18th Sep , 2021

Kocha Mkuu wa klabu ya Arsenal 'Washika mitutu wa jiji la London', Mikel Arteta amefunguka na kusema anaumia sana kuona wapinzani wake wanashiriki michuano ya klabu bingwa Ulaya muda ambao Arsenal imetimiza miaka minne mfululizo bila kushiriki michuano hiyo.

Picha ya kocha Mikel Arteta

Arteta amesema "Unaniumiza sana, siku chache zilizopita nilivyowasha Luninga na kuona timu nyingine zikishiriki michuano hiyo na sio Arsenal".

Arteta ameyasema hayo akiwa anazingumza na Wanahabari kuelekea mchezo wake wa EPL ugenini dhidi ya Burnley utakaochezwa Saa 11:00 Jioni ya leo Septemba 18, 2021 kwenye dimba la Burnley la 'Turf Mor'.

Kuelekea kwenye mchezo huo, Arsenal itawakosa nyota wake watatu kutokana na sababu mbalimbali, Nyota hao ni Granit Xhaka anayetumikia adhabu ya kuoneshwa kadi nyekundu, Mohammed Elneny anayesumbuliwa maumivu ya Misuli ilhali Rob Holding anamaumivu ya goti.

Kwa upande wa Burnley, kocha wake Sean Dyche amesema hatomuharakisha kumchezesha mchezaji wake mpya Maxwel Cornet licha ya kuwa na mchezo huo ni  mkubwa mbele yake.

 Sean ataingia kwenye mchezo huo akiwa na ari nzuri baada ya kusaini kandarasi ya miaka 4 kusalia Turf Mor hadi mwaka 2025 huku akiwa kocha aliyehudumu EPL kwa muda kulinganisha na makocha waliopo sasa, muda wa miaka 9.

Arsenal ambayo haijamfunga Burnley kwenye michezo mitatu ya mwisho, ipo nafasi ya 17 ikiwa na alama 3 baada ya kucheza michezo 4 ilhali Burnley ipo nafasi ya 19 wakiwa na alama 1 licha ya kucheza michezo 4.

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma