Carlos Alberto, Nahodha wa zamani wa Brazil, akiwa amenyanyua kombe la Dunia 1970
Alberto, anakumbukwa, kwa kufunga mojawapo ya mabao mazuri zaidi duniani katika historia ya Kombe la Dunia katika mechi ya fainali dhidi ya Italia mwaka 1970, baada ya kuwachenga mabeki na kufunga kwa mkwaju mkali.
Beki huyo wa kulia Carlos Alberto alicheza mechi 53 katika timu ya taifa ya Brazil na kushinda mataji ya nyumbani akiwa na Fluminense na Santos alikocheza jumla ya mechi 400.


