
Dismas Ten na Amri Said
Dismas amempa heshima hiyo Amri Said ambaye katika mchezo wake wa kwanza tu tangu awe kocha wa Biashara United alishinda 2-1 dhidi ya Mbeya City, hivyo Ten amekiri kuwa Amri Said ameibadilisha timu hiyo.
''Tumepangwa kucheza nyumbani dhidi ya Biashara United, mchezo utakuwa mgumu ukizingatia mabadiliko ya benchi la ufundi ambayo wamefanya Biashara lakini pia lazima uzingatie kuwa waliifunga timu gani'', ameongeza Dismas.
Yanga ambao ni mabingwa wa michuano hiyo msimu wa 2015/16 wametinga raundi ya 4 baada ya kuwatoa Tukuyu Stars ya Mbeya kwa mabao 4-0 huku Amisi Tambwe akifunga Hat-trick.
Amri Said aliifundisha Lipuli FC msimu wa 2017/18 na kuisaidia kumaliza katika nafasi ya 7 ikiwa na alama 38. Msimu huu aliuanza na Mbao FC kabla ya kuachana nayo mwezi Desemba na kujiunga na Biashara United.