Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanaume hawa hatarini kupata vipara

Jumapili , 15th Jan , 2023

Wanaume wanaopendelea kutumia vinywaji vyenye sukari kila siku wapo hatarini kupoteza nywele zao na kuwa wenye viapara.

Kipara

Utafiti huo umefanywa na Chuo Kikuu cha Tsinghua cha nchini China, ambao umeeleza kuwa wanaume wanaopoteza nywele na kuwa vipara kwa siku za hivi karibuni wanahusishwa na unywaji wa vinywaji vingi vyenye sukari.

Utafiti huo uliangalia data kutoka kwa wanaume zaidi ya 1,000 wa China, wenye umri wa miaka 18 hadi 45, kuanzia Januari hadi Aprili 2022 ili kulinganisha tabia za maisha zinazoripotiwa na upotezaji wa nywele.

Waligundua kuwa upotezaji wa nywele ulikuwa karibu ya 30% zaidi ya wanaume ambao walikuwa na tabia ya kila siku ya kunywa kinywaji chenye sukari kama vile vinywaji baridi, juisi, vinywaji vya kuongeza nguvu, vinywaji vya michezo, kahawa na chai iliyotiwa ambapo ni sawa na lita moja hadi tatu kwa wiki.

Wanaume ambao waliripoti kuwa na zaidi ya kinywaji kimoja cha sukari kwa siku walikuwa na uwezekano mkubwa wa kupoteza nywele kwa 42% zaidi ikilinganishwa na wale ambao hawakuwahi kunywa vinywaji vya sukari.

Watafiti pia waligundua kuwa wengi wa washiriki wa utafiti walikunywa angalau baadhi ya vinywaji vyenye sukari katika lishe yao ya kila siku na karibu nusu waliripoti kuwa na vinywaji vyenye sukari zaidi ya mara moja kwa siku.

Utafiti huo umeainisha kwamba tabia za wanaume kunywa vinywaji vyenye sukari sio sababu pekee za upotezaji wa nywele, bali kuna sababu zingine kama vile lishe duni, masuala ya afya, mkazo na matatizo ya afya ya akili.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi