Jumatatu , 19th Aug , 2019

James Banes (41) na Victoria Banes (38 ) ni ndugu wawili wa familia moja pia ni wapenzi kutoka New Jersey Marekani, wameshinda shauri la mahakama kuhusu kufunga ndoa.

Ndugu hao wameshinda shauri hilo baada ya kukaa miaka 10 kupambania kuhusu kupitishwa kwa sheria hiyo kwa kaka na dada kuona wenyewe kwa wenyewe.

James Banes ambaye ni kaka wa familia hiyo amesema, "alikuwa anaishangaa mahakama kukubali mtu kufunga ndoa na binamu yake na si mtu na dada yake ilihali kuwa hata Adam na Hawa walifanya hivyo kwa nini leo isiwe kwa sisi ndugu".

Pia Victoria Banes naye ameendelea kusema muda wote walikuwa na ndoto ya kuwa na familia kubwa na ndoto hizo zinakuja kuwa kweli baada ya kushinda kesi hiyo na kwa sasa ni mjamzito anategemea watoto mapacha.

Baada ya kushinda kwa kesi hiyo ndugu hao wamesema walifurahi sana kusikia hivyo na kupitia wao, watawahamasisha mamilioni ya wamerakani kuwa na mahusiano na ndugu zao.