Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manyanya awatolea uvivu wanafunzi wanaojiuza

Ijumaa , 2nd Dec , 2016

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandisi Stella Manyanya amewatolea uvivu wanafunzi wa elimu ya juu wanaodaiwa kujiuza kwa madai ya kukosa mkopo na kusema kuwa, wanafunzi hao wana tatizo la ziada na siyo mkopo pekee.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandisi Stella Manyanya akiwa Kikaangoni

 

Manyanya amefunguka hayo Jumatano hii alipokuwa katika kipindi cha KIKAANGONI kinachoruka LIVE kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV, ambapo alisema kukosa mkopo hakuwezi kuwa sababu ya mwanafunzi kufanya matendo yaliyo kinyume na maadili na kusisitiza kuwa hiyo ni tabia ya mtu na kwamba serikali isitwishwe mzigo huo.

"Kama kweli kuna wanafunzi wa kike wanaojiuza kwa kukosa mkopo, wana tatizo la ziada, haiwezekani hiyo iwe sababu, maana kama ni kukosa mkopo wanafunzi wengi wanakosa, mbona wengine hawafanyi hivyo? na je wanafunzi wa kiume wanaokosa mkopo wao wauze nini?" alihoji Manyanya na kuwaonya waache mara moja tabia hiyo.

Pia ametumia nafasi hiyo kuwaasa wazazi kuwajibika katika malezi ya watoto wao na kuwafundisha maadili mema ili wasiwe na tabia za aina hiyo ambazo ni kinyume na mila za kitanzania, pamoja na kuwagharamia masomo yao.

"Wazazi lazima wajue wajibu wao ni pamoja na kuwasomesha waototo wao, wasitegemee kila kitu serikali, serikali ina nafasi yake na wazazi wana nafasi yao, ni lazima wawajibike"

Amesema kwa wanafunzi waliokosa mikopo na hawana uwezo watafute njia nyingine ikiwa ni pamoja na kutumia ndugu jamaa na marafiki kwa kuwa hakuna mwaka ambao wanafunzi wote walipata mkopo huku akiwataka watambue kuwa mkopo ni msaada na ni kitu cha ziada hivyo si cha kutegemea sana.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu