Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bao la Ajibu lilikuwa halali - Msuva

Alhamisi , 24th Nov , 2016

Bao alilofunga mshambuliaji wa Simba Ibrahim Ajibu katika mechi dhidi ya Yanga Oktoba 01, mwaka huu limeendelea kuzusha mjadala ambapo winga machachari wa Yanga Simon Msuva amesema lilikuwa ni bao halali.

Ibrahim Ajibu - Mshambuliaji wa Simba

Bao hilo lilikataliwa na waamuzi kwa madai kuwa Ajibu alikuwa ameotea kabla ya kufungwa. 

Akizungumza na mashabiki wa soka nchini kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachoruka LIVE kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV, Msuva amesema kwa mtazamo hakuona tatizo lolote kwa bao lile, na kwamba alishangazwa na maamuzi ya mwamuzi kudai kuwa Ajibu alikuwa ameotea.

"Wakati bao likifungwa mimi nilikuwa bado sijaingia, nilikuwa benchi, kwaiyo kwa pale uwanjani ni ngumu sana kuwa na uhakika kama aliotea au alikuwa hajaotea, lakini tulipokuja kuangalia marudio kwenye video niliona vizuri, wakati pasi ile inapigwa kwa Ajibu alikuwa hajaotea na alifunga bao zuri ambalo kwa mtazamo wangu ni bao halali, lakini kwa kuwa waamuzi wanaona vizuri zaidi yangu, walikuwa sahihi pia kulikataa kwa kuwa wao ndiyo wenye maamuzi". Alisema Msuva.

Simon Msuva akiwa Kikaangoni, EATV

Akizungumzia bao lililofungwa na Tambwe katika mchezo ule, Msuva amesema pia lilikuwa ni bao halali kwa kuwa mpira ndiyo ulifuata mkono wa Tambwe kabla hajafunga, na kwa kuwa mwamuzi aliamua liwe bao, kwake yeye ni bao halilali. 

Kuhusu bao la la kusawazisha ambalo Simba walilipata kupitia kwa Shiza Kichuya dakika za mwisho, Msuva alisema bao lile liliwaumiza kabisa na kuwatoa kwenye mchezo kwa kuwa ni jambo ambalo hawakutegemea na kwamba hadi dakika ile ya 87 walikuwa wanajua kuwa tayari wameondoka na ushindi licha ya kukiri kuwa Simba walibadilika dakika za mwisho na kuongeza ushindani.

Alisema yeye na wachezaji wenzake Yanga wamejipanga vizuri na watahakikisha wanapata ushindi katika mchezo wa marudiano dhidi ya Simba utakaopigwa Februari mwakani huku akisisitiza kuwa Yanga ina nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu Bara kwa mara ya 3 mfululizo.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali