Alhamisi , 16th Oct , 2014

Wyre, staa wa muziki kutoka nchini Kenya amefanikiwa kupata haki ya kufanyia kazi upya ya nyimbo kali kabisa kabisa za msanii mkongwe wa Muziki wa kiafrika, Kanda Bongoman.

Kanda Bongo Man na Wyre

Kupitia nafasi hii, Wyre anatarajiwa kutoka na kazi ambayo imeboreshwa na ina vionjo vya kisasa kutoka rekodi kama Inde Monie ambayo iliweza kutikisa mawimbi vilivyo katika kipindi cha nyuma.

Wyre amekuwa na rekodi ya kuzitendea haki ngoma za zamani ambazo anazirudia, kitu ambacho kinawapatia mashabiki hamu kubwa zaidi kuona kile atakachofanya kutoka kazi za Kanda Bongoman.