Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waziri Nape kutikisa anga la Afrika Mashariki leo

Jumamosi , 10th Dec , 2016

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Nape Nnauye leo anatarajiwa kutikisa anga la Afrika Mashariki pale atakapoongoza utoaji wa tuzo kubwa za muziki na filamu katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akicharaza gita

Nape Moses Nnauye anaingia kwenye historia ya ulimwengu wa burudani katika ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa serikali kuongoza na kutoa tuzo katika tuzo ambazo ndiyo zinaanza kutolewa mwaka huu wa 2016.

Huyu ni waziri wa kwanza katika serikali ya awamu ya tano kuongoza wizara hiyo, na katika kipindi cha takriban mwaka mmoja ameonesha ukaribu wa hali ya juu na wasanii, huku akianzisha harakati za kukabiliana na uharamia wa kazi za sanaa kwa kusambaratisha viwanda vidogo ambavyo vimekuwa vikitegeneza na kusambaza kazi feki za wasanii nchini.

Mbali na jitihada hizo, Nape pia ni mdau mkuubwa wa sanaa, kwa maana ya kuwa msanii mwenye uwezo mkubwa wa kucharaza gitaa na kuimba.

Nape anatarajiwa kukabidhi tuzo ya heshima kati ya tuzo 10 zitakazotolewa leo.

Vipengele vingine vinavyowaniwa ni pamoja na Mwanamuziki Bora wa Kiume, Mwanamuziki Bora wa Kike, Wimbo Bora wa Mwaka, Video Bora ya Mwaka, Kundi Bora la Mwaka, Mwanamuziki Bora Chipukizi, Muigizaji Bora wa Kiume, Mwanamuziki Bora wa Kike, pamoja na Filamu Bora ya Mwaka.

Wasanii mbalimbali watawasha moto kwenye stage, ambao ni pamoja na Barnaba Boy, Maurice Kirya kutoka Uganda, rapa mkali Darassa, Shetta, Vanessa Mdee, Wahu kutoka Kenya, Lady JayDee, Ali Kiba aka King Kiba pia Madansa wakali wa shindano la kudansi la Dance100% 2016, washindi Team Makolokocho, Clever Boys pamoja na D.D.I

Wahi tiketi yako sasa kwa utaratibu ufuatao.

 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu