Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wasanii waipa shavu ‘Konyagi’ kuthamini wanawake

Jumanne , 9th Mar , 2021

Katika kuadhimisha kusherehekea siku ya Wanawake Duniani 2021, wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini wamekipongeza kinywaji cha Konyagi kwa kuwapa fursa ya kuthamini ujasiri, ushupavu na uthubutu wa wanawake ambao wamejitoa katika mafanikio ya kazi zao za kimuziki

Msanii Mwasiti

na kuwajenga katika Maisha kiujumla.

Mmoja wa wasanii hao, John Simon Mseke, au maarufu kama Joh Makini, ‘Mwamba wa Kaskazini’, ameishukuru Konyagi kwa fursa iliyompa ya kumzungumzia mwanamke ambaye anaamini amekuwa na mchango mkubwa katika maisha yake na amesema mama yake mzazi ndio kila kitu kwake na anabaki kuwa mwanamke wa nguvu katika maisha yake.

Joh Makini, mzaliwa wa jijini Arusha, ambaye anajulikana kwa wimbo kama "Popote Chochote" anasema mama yake amekuwa ndio kioo chake tangu akiwa mtoto mpaka sasa akiwa mwanamuziki maarufu.

‘Siwezi kumaliza maneno nikiamua kumzungumzia mama huyu shupavu,” Amesema Joh. “Mimi mwenyewe ni mzazi pia, hivyo najua changamoto alizopitia mama yangu wakati nikiwa tumboni, aliponizaa na wakati akinilea.” anasema mkali huyo ambaye pia ni mwanachama hai wa kundi la "Weusi" kutoka Arusha.

Msanii Joh Makini

Naye Juma Jux, maarufu kama ‘African Boy’ ambaye ni miongoni mwa wasanii wanaosemekana kulipwa hela nyingi katika show zake,amesema mama yake amekuwa na mchango mkubwa katika safari yake ya kimuziki iliyokuwa na vikwazo vingi vya kukatisha tamaa.

Jux, anayeshirikiana na wanamuziki mbalimbali katika nyimbo zake akiwemo Diamond Platnumz aliyeshirikiana naye katika wimbo unaoitwa ‘Sugua” na ule wa ‘Juu’ alioshirikiana na mpenzi wake wa zamani, Vanessa Mdee, anasema kuna watu wake kadhaa wa karibu, wakiwemo wa familia yake waliomkatisha tama wakati anaanza muziki, lakini mama yake alimwambia anaweza.

“Mama alinifundisha maisha, namna ya kuwajali wanawake wengine na watu wote wanaonizunguka. Licha ya kuwa peke yake, alinipa malezi bora na kunilea,” anaongeza Jux.

“Kwangu mimi, mama yangu ni jasiri ‘ hero’ na kupitia siku hii muhimu, nawatakia wanawake wote heri ya kusherehekea sikukuu ya wanawake Duniani” alimalizia kusema Jux huku akishukuru Konyagi kwa kumpa fursa ya kutambua mchango wa mwanamke huyo muhimu kwake maishani.

Msanii Jux

Siku ya Wanawake Duniani imegusa kila mtu duniani kutokana na mchango wa akina mama, sio tu katika malezi na kujenga familia bora, bali pia kushiriki shughuli za kiuchumi katika nyenzo na nyanza mbalimbali, ikiwemo kufanya shughuli ambazo zimekuwa zikifanywa na wanaume kama vile udereva, ufundi na nyinginezo nyingi. Konyagi pia imetoa chupa yenye nembo maalumu ya mwanamke aliyeinua mikono kama kiashiria cha kutambua umuhimu wa mwanamke katika jamii.

Katika wasanii wengine waliopata fursa ya kutambua Wanawake muhimu katika Maisha yao ni Msanii Mwasiti ambaye amemtambua Angelique Kidjo kama mwanamke aliyempa ujasiri kwa kazi zake za muziki na mchango katika jamii.

Msanii Snura Mushi pia ametambua watu watatu ambao ni bibi yake, muigizaji Monalisa pamoja na muimbaji wa muziki wa taarab Sabaha Salum.

Maelezo ya wasanii hawa yamepewa nguvu na kampuni ya Tanzania Distilleries Limited , inayotengeneza kinywaji cha Konyagi katika kutambua ujasiri, weledi, ushupavu na uthubutu wa mwanamke katika kujiletea maendeleo kupitia shughuli anazofanya katika jamiii inayomzunguka.

Meneja Chapa wa Konyagi inayotengenezwa na kampuni ya Tanzania Distilleries Limited, Pamela Kikuli amesema kinywaji hicho ni kile kile kwa ladha na ubora lakini ameona kuna umuhimu wa kutambua umuhimu wa Wanawake kwa kuweka nembo maalum kwa kipindi hiki maalum.

Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa tarehe 8 Machi ya kila mwaka. Siku hiyo ilianza kuadhimishwa tarehe 8 Machi 1975 baada ya Umoja wa Mataifa kuridhia siku hii kutumika kama siku rasmi ya kuikumbusha dunia juu ya haki za wanawake.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto