Alhamisi , 24th Jun , 2021

Hit maker wa Mr President, Rapper Roma Mkatoliki kabla ya kuanza kusikika na kazi zake zilizopikwa Tongwe Records alianza kurekodi wimbo wake wa kwanza 2004 Tanga kwa shilingi elfu 70 na uliitwa ‘Masharti ya Mganga’.

Picha ya Msanii

Wimbo huo ulirekodiwa katika studio za msanii na mtayarishaji wa muziki  marehemu Abel Motika (Mr. Ebbo) huko mkoani Tanga na aliwashirikisha Kassim na Dickson Msami ambaye aliimba korasi (chorus) katika wimbo huo.

Dickson Msami ambaye kwasasa ni mtangazaji wa East Africa Radio na Tv ndiye aliyempeleka studio za Motika kipindi hicho nakulipia gharama hizo kwa ajili ya kurekodi wimbo licha ya kuwa haukuwahi kutoka.