Jumatano , 30th Apr , 2014

Msanii wa muziki wa injili anayefanya vizuri nchini Kenya, Ringtone ameripotiwa kuwa katika mkakati wa kupanua soko la muziki wake huko Afrika Magharibi, ambapo staa huyu amefika Nigeria na kukutana na DJ Gosporella ambaye ni mdau mkubwa wa muziki.

Ringtone

Ringtone ametajwa kutengeneza mpango wa manufaa kwa muziki wa Kenya na DJ huyu, ambapo kwa pamoja watasaidiana kuupatia muziki kutoka Kenya nafasi ya kuchezwa zaidi huko Nigeria, na pia kutengeneza nafasi ya muziki wa Nigeria kuchezwa nchini Kenya.

Mkakati huu wa Ringtone, unatarajia kusaidia kwa kiasi kikubwa kueneza kazi za wasanii kutoka Kenya katika soko kubwa kabisa la muziki huko Afrika ya Magharibi.