Jumatatu , 19th Jan , 2015

Msanii wa muziki wa Injili wa nchini Kenya, Ringtone amesema kuwa ana wasiwasi mkubwa juu ya kushuka kwa sanaa ya muziki wa Injili nchini humo kutokana na kuona kuwa haupewi msikumo kama inavyotakiwa.

msanii wa muziki wa injili nchini Kenya Ringtone

Ringtone amesema kuwa, katika tasnia hiyo kuna changamoto kubwa, pia kwa upande wa upangaji wa bei ya kazi zao ambao pia kama hautaangaliwa sasa, utasababisha kufa kwa muziki huo.

Kwa upande mwingine, Staa huyu ambaye pia hivi karibuni alikuwa anakabiliwa na tuhuma za kudhulumu gari, amesema kuwa gari analodaiwa kudhulumu ni la kwake kihalali kutokana na mteja aliyemuuzia kushindwa kukamilisha malipo yake kwa wakati.