Jumatatu , 11th Aug , 2014

Wasanii Radio na Weasel kutoka Uganda, wameanza kwa kishindo kuendesha shughuli za muziki wao nje ya mipaka ya Uganda, bila usimamizi wa meneja Jeff Kiwa, kwa kufanya onesho kali huko Dubai mwishoni mwa wiki.

wasanii wa nchini Uganda Mose Radio & Weasel

Wasanii hawa baada ya kufanikisha shughuli hii, wamefunguka kueleza kuwa, wana furaha kwa kuweza kuwaondoa panya katika makabati yao, maneno ambayo yanaonekana kuwa dongo la moja kwa moja kwa timu ya Jeff aliyekuwa anasimamia kazi zao.

Jeff Kiwa amekuwa akiwasimamia Radio na Weasel kwa miaka kadhaa sasa, akionekana ndiyo msingi wa kuwapatia wasanii hawa show kubwa za nje ya nchi kabla ya kugombana mwanzoni mwa mwaka huu.