
Iryn Namubiru
Iryn amesema haya baada ya kuulizwa ha moja ya ndugu zake wa karibu kuhusiana na swala la yeye kuolewa tena, swali ambalo lilionekana dhahiri kugusa hisia za mwanadada huyu na kumkumbusha machungu, huku akionyesha dhahiri kuwa hayupo tayari kutoa taarifa zaidi juu ya swala hili zito kwa upande wake.
Iryn kwa sasa anatajwa kuwa katika ugomvi mwingine wa mapenzi baada ya kugundua kuwa mpenzi aliyenaye sasa, ana mahusiano pia na mwanadada anayefahamika kwa jina Safia Kodet ambaye kwa sasa amegeuka kuwa hasimu wake mkubwa.