Jumatano , 30th Sep , 2015

Msanii wa muziki Muki kutoka kundi la Makomando, ametoa ya moyoni dhidi ya mashabiki ambao wamekuwa wakishambulia wasanii kutokana na misimamo yao ama kutumbuiza katika majukwaa ya kisiasa, akisema kuwa wanafanya hivyo kwa nia ya kutumbuiza tu.

Msanii wa muziki Muki kutoka kundi la Makomando

Kwa niaba ya mwenzake Fredywine, Muki ameiambia eNewz kuwa kama msanii, anaona ni vigumu na ni aibu kwa wasanii kubaki nyuma katika kipindi kama hiki cha uchaguzi, mtazamo ambao wengine wanaupinga vikali.

Katika wakat huu ambao wasanii wamegawanyika kimtazamo kuhusiana na kujihusisha kisiasa, wengine wakiona ni sawa huku wengine wakijiweka kando, huu ndio msimamo wa Muki, Makomando kwa ujumla kuhusiana na baadhi ya wasanii ambao wanajihusisha na siasa.